
Global Services High Targets
LEADERSHIP – ENTREPRENEURSHIP – VOLUNTEERING
BRELA ID No: 465066, TIN:
BAKWATA ID: BKT /MDRS/O2O/O1O15
0768649111 – 0675103790 – 0777496444 – 0772496444
Email: gshcourt@gmail , uddgshcourt@gmail
TANZANIA DAR es SALAAM, UBUNGO KWEMBE, MLOGANZILA
​
UBUNGO, KWEMBE, MLOGANZILA

HUDUMA BILA MALIPO KWA WANAFUNZI


MUSTAKBALI NA HATMA VIZAZI KATIKA JAMII YETU UMO MIKONONI KWA VIJANA WETU . LEO HII ASILI MIA KUBWA SANA YA VIJANA WAISLAM WAMEBAKI WAKIJINASIBU NA UISLAM HALI YA KUWA WAPO MBALI NA UISLAM HALISI KIUTENDAJI NA KIITIKADI, JAMBO HILI LIMECHANGIWA NA HALI YA WATU WAZIMA KUKAA MBALI NA VIJANA. KUNA HAJA KUBWA YA KUANZISHA JUHUDI KATIKA MAENEO MBALI MBALI KWA AJILI YA KULINDA VIJANA WETU NA MAMBO YANAYO WAWEKA KANDO NA DINI WAKIWA WAO HAWANA HABARI KABISA. HIVYO SISI TAYARI NI SEHEMU YA JUHUDI HIZO INGAWA CHANGAMOTO ZA NDANI NA NJE YA JAMII YETU NI KUBWA SANA KULIKO UWEZO WETU. HATA HIVYO TUTAENDELEA KADRI ATAVYO TUWEZESHA ALLAH.
VIJANA NDIO JAMII
01
FIQHU NA ITIKADI
Kuwafundisha mambo muhimu katika dini kiasi waishi maisha yao wakuwa waelewa majukumu yao kwa mola wao na jamii kwa jumla, kwa mujibu wa maelekezo ya Uislm
03
UONGOZI BORA NA SALAAMA
Huwa tunatoa mafunzo ya utawala, uendeshaji na uongozi kwa vijana wetu. Hii ni baada ya kubaini kuwa vijana wetu wamekuwa wa kiharibikiwa katika uongozi wa umoja wa vijana waislam huko mashuleni.
05
MAFUNZO YA SAIKOLOJIA
Kutokana na umuhimu wa saikolojia kwa viumbe walio hai, tumekuwa tukitoa mafunzo hayo kwa vijana wetu ili watape uelewa wa mambo yanayo jiri katika mazingira wanako ishi wao. Jambo litakalo wasaidia kuepuka "unenguaji wa ngoma sio zao".
02
MAISHA YA BAADA YA MASOMO
Uhalisia wa vijana wengi wakiwa masomoni huwa wapo mbali na kutambua kuwa ndoto zao za maisha zinaweza kuishia hewani na kubaki kuwa zilikuwa ni ndoto za alinacho. Jambo hili huchangiwa sana na uhalisia wa maisha walio yaishi vijana wetu tokea safari yao ya kutafuta elimu.
Hivyo tuliona haja ya kuwajuza wasio yajua kuhusi uhai na maisha.
04
TUITION
Utatuzi wa kitaaluma kwa wanafunzi walio na matatizo katika masomo yao. Tunapanga program kwa mujibu wa viwango vya kitaaluma. Programu hizo ni kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari tu. Mafunzo hayo ni bila malipo. Hata hivyo zipo taratibu za kufuatwa ili kujiunga,
06
KUENDESHA MIJADALA
Tunayo programu ya kuendesha mijadala (debats) ili kukuza viwango vya usimamishaji wa hoja kwa vijana wetu kila inapo wabidi kufanya hivyo maishani mwao.